Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mbossa leo Jumapili amesema kwa kawaida Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) hukusanya tozo kutokana na meli 90 zinazohudumiwa kwa mwezi na uboreshaji utakapofanyika kupitia kampuni ya DP World wataweza kuhudumia meli 130. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Akitoa taarifa kuhusu mikataba mitatu iliyosainiwa leo Ikulu jijini Dodoma, amesema mapato yaliyokuwa yanakusanywa na TRA yataongeza kutoka Sh tirilioni 7.8 ambazo zinakusanywa eneo la bandari peke yake kwa mwaka 2021/2022 hadi kufikia trilioni 26.7 itakapofika mwaka 2032.
Amesema ushirikishwaji wa sekta binafsi sio kitu kipya katika mkataba huo ambao ni wa aina yake.
Amesema mkataba huo umezingatia changamoto za serikali kupitia mkataba wa awali kati ya TPA na TICTS ambao ulikoma tarehe 31 Disemba mwaka 2022.
Leave a comment