Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa TRA ilishindwa kukusanya Sh. 17.28 Bil, 2019/20-CAG
Habari za Siasa

TRA ilishindwa kukusanya Sh. 17.28 Bil, 2019/20-CAG

Spread the love

 

RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2019/2020, imebaini Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ilishindwa kukusanya ushuru wa forodha Sh. 17.28 bilioni, kutokana na sababu mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Alhamisi tarehe 8 Aprili 2021, jijini Dodoma na CAG, Charles Kichere, wakati akitoa muhtasari wa ripoti hiyo, iliyowasilishwa bungeni.

Akielezea changamoto za TRA, CAG Kichere amesema katika kipindi hicho, TRA ilishindwa kukusanya ushuru wa forodha wa Sh. 5.14 Bilioni wa biadhaa zilizopita kwenda nje ya nchi.

Charles Kichere, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

Bidhaa hizo zilipitishwa katika mipaka ya Tunduma, Kasumulu, Rusumo, Kabanga, Mutukula, Namanga, Holili na Kigoma.

“Katika ukaguzi wangu wa bidhaa zinazopita nchini kuelekea nchi jirani, kupitia mipaka ya forodha kwa kuangalia mfumo wa TANCIS na nyaraka za kusafirishia, sikuthibitisha kuwa bidhaa zenye makadirio ya kodi ya forodha Sh. bilioni 5.14 zilitoka nchini,” amesema CAG Kichere.

Mbali na bidhaa hizo kupitishwa nje ya nchi bila kulipiwa ushuru wa forodha, CAG Kichere amesema, TRA ilishindwa kukusanya ushuru wa forodha wa Sh. 12.14 Bilioni wa mafuta yaliyopitiliza muda wake, ambayo yalipaswa kwenda nchi jirani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!