Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa TRA ilishindwa kukusanya Sh. 17.28 Bil, 2019/20-CAG
Habari za Siasa

TRA ilishindwa kukusanya Sh. 17.28 Bil, 2019/20-CAG

Spread the love

 

RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2019/2020, imebaini Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ilishindwa kukusanya ushuru wa forodha Sh. 17.28 bilioni, kutokana na sababu mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Alhamisi tarehe 8 Aprili 2021, jijini Dodoma na CAG, Charles Kichere, wakati akitoa muhtasari wa ripoti hiyo, iliyowasilishwa bungeni.

Akielezea changamoto za TRA, CAG Kichere amesema katika kipindi hicho, TRA ilishindwa kukusanya ushuru wa forodha wa Sh. 5.14 Bilioni wa biadhaa zilizopita kwenda nje ya nchi.

Charles Kichere, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

Bidhaa hizo zilipitishwa katika mipaka ya Tunduma, Kasumulu, Rusumo, Kabanga, Mutukula, Namanga, Holili na Kigoma.

“Katika ukaguzi wangu wa bidhaa zinazopita nchini kuelekea nchi jirani, kupitia mipaka ya forodha kwa kuangalia mfumo wa TANCIS na nyaraka za kusafirishia, sikuthibitisha kuwa bidhaa zenye makadirio ya kodi ya forodha Sh. bilioni 5.14 zilitoka nchini,” amesema CAG Kichere.

Mbali na bidhaa hizo kupitishwa nje ya nchi bila kulipiwa ushuru wa forodha, CAG Kichere amesema, TRA ilishindwa kukusanya ushuru wa forodha wa Sh. 12.14 Bilioni wa mafuta yaliyopitiliza muda wake, ambayo yalipaswa kwenda nchi jirani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!