Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania kuwa mwenyeji mkutano wa wahisani
Habari Mchanganyiko

Tanzania kuwa mwenyeji mkutano wa wahisani

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Legal Services Facility (LSF), Lulu Ng'wanakilala
Spread the love

 

TANZANIA inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano wa nane wa mtandao unaojishughulisha na masuala ya utoaji misaada kwa jamii, East African Philanthropy network (EAPN), unaotarajiwa kufanyika visiwani Zanzibar Juni, 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungunza na waandishi wa habari kwa njia ya mtandao, Afisa Mtendaji Mkuu wa EAPN, Evans Okinyi amesema mkutano huo utafanyika Zanzibar kwa siku mbili, kuanzia tarehe 28 hadi 30, Juni 2023, ambapo utajumuisha wataalam na taasisi za masuala ya uhisani zaidi ya 300.

Okinyi amesema lengo la mkutano huo ni kujadili ubunifu utakaosaidia kuhamasisha utekelezaji mipango ya uhisani pamoja na kutatua changamoto zake.

Afisa Mtendaji huyo wa EAPN, amesema mkutano huo hautanufaisha sekta ya uhisani peke yake, bali utahamasisha mabadiliko ya mifumo ili kuongeza jitihada za utoaji hisani kwa jamii.

“Haijalishi ni namna gani tunauangalia mkutano huu. Ukweli ni kwamba muingiliano wa kijamii uliopo katika ulimwengu wa sasa unahitaji jamii inayoweza kufanya kitu ama kuelewa mambo kwa namna nzuri. Tunalenga pia kuwezesha zaidi wale ambao hawawezi kusema kwa kubadilisha mitazamo yao kifikra ili kuyaangalia mambo ambayo pengine yanaonekana kuwa hayawezekani kuwa yanawezekana,” amesema Okinyi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Legal Services Facility (LSF), Lulu Ng’wanakilala, amesema Shirika lake linaona fahari kuratibu mkutano huo kwa niaba ya wadau wa EAPN

“Mkutano huu ni jukwaa la kubadilishana uzoefu pamoja na kufanya tathmini ya pamoja ili kubuni njia bora za jamii kufanya hisani na kuwekeza kwa ajili jamii na wadau mbalimbali barani Afrika. Hivyo, nawaomba mashirika yote ya uhisani nchini, sekta binafsi, serikali, CSOs na wadau wengine muhimu wa maendeleo kuungana pamoja katika mkutano huu muhimu,” amesema Ng’wanakilala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!