SOKO la wafanyabiashara wadogo wadogo ‘Wamachinga’ lililopo Mbagala Rangi Tatu jijini Dar es salaam limeungua kwa moto usiku wa kuamkia leo asubuhi tarehe 13, 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa uchunguzi wa chanzo cha moto huo bado unaendelea.
Hata hivyo, imeelezwa kuwa sehemu iliyoathirika zaidi ni ya wauza mitumba ambapo baadhi ya bidhaa zao zikiteketea kwa moto, lakini hakuna aliyeripotiwa kupoteza maisha wala kujeruhiwa.
Aidha, taarifa za awali zinaeleza kuwa chanzo cha moto huo kinadhaniwa kuwa ni hitilafu ya umeme na jeshi la zima moto lilifika na kuukabiliana moto huo.
Leave a comment