Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Simba Vs Yanga: TFF yaomba radhi, yatoa maagizo
Habari Mchanganyiko

Simba Vs Yanga: TFF yaomba radhi, yatoa maagizo

Ofisi za TFF
Spread the love

 

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limewaomba radhi wadau wa michezo, kwa tukio lililotolea jana Jumamosi, tarehe 8 Mei 2021, la kuahirishwa mchezo wa ligi kuu, kati ya watani wa jadi, Simba dhidi ya Yanga. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Mchezo huo, uliahirishwa baada ya Yanga kupinga mabadiliko ya muda wa mchezo huo, kutoka saa 11:00 jioni wa awali hadi saa 1:00 usiku.

TFF ilitangaza mabadiliko hayo takribani saa 3 kufika saa 11:00 mchezo kuanza ikiwa ni kinyume na kanuni ya 10(15) ya ligi hiyo inayotaka mabadiliko hayo, yafanyike saa 24 kabla ya mchezo.

TFF iliahirisha mchezo huo uliokuwa uchezwe Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam hadi hapo baadaye.

Leo Jumapili, Cliford Ndimbo, Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, ametoa taarifa akisema, suala hilo linaendelea kushughulikiwa.

“TFF inapenda kuomba radhi kwa wadau wote, waliolipa viingilio kuingia uwanjani, waliokuwa wakisubiri kuangalia kwenye televisheni, kusikiliza redioni na watoa huduma mbalimbali,” amesema Ndimbo

Amesema, TFF imetoa maelekezo kwa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), kutoa taarifa ya kina kuhusu kuahirishwa kwa mchezo huo.

Pia, kushughulikia hatma ya wapenzi wa mpira wa miguu waliolipa viingilio kuingia uwanjani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!