Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Rais Samia amkabidhi Kikwete nyumba ya kuishi
Habari Mchanganyiko

Rais Samia amkabidhi Kikwete nyumba ya kuishi

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemkabidhi nyumba ya kuishi, Rais mstaafu, Jakaya Mrisho Kikwete. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Ni iliyojengwa katika Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam ambayo imejengwa na Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).

Nyumba hiyo ni utekelezaji wa kifungu namba 12 cha Sheria ya mafao ya hitimisho la kazi kwa viongozi wa siasa, sura ya 225 na marejeo ya mwaka 2020 ambayo pamoja na stahili zingine za matunzo ya viongozi wakuu wastaafu inaelekeza kuwa Rais anayestaafu anastahili kujengewa nyumba ya kuishi yenye hadhi ya Rais.

Mara baada ya kukabidhi nyumba hiyo, leo Jumapili, tarehe 9 Mei 2021, Rais Samia amempongeza Kikwete kwa kupata makazi hayo na amemhakikishia, Serikali itaendelea kumtunza yeye na viongozi wengine wastaafu kama inavyoelekezwa katika sheria.

Amebainisha Serikali itafanyia kazi uboreshaji wa sheria hiyo pamoja na kuhakikisha wajane/wagane wa viongozi wanatunzwa.

Rais Samia amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa kuanza maandalizi ya kutimiza haki zote anazostahili aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati John Pombe Magufuli.

Kwa upande wake, Waziri Mchengerwa amesema nyumba hiyo ni ya tatu kukabidhiwa ikitanguliwa na nyumba ya Rais Mstaafu Hayati Benjamin William Mkapa na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi na kwamba nyumba ya Baba wa Taifa Hayati Mwaimu Julius Kambarage Nyerere ilijengwa na kukabidhiwa kwake na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Katika shukrani zake, Rais Mstaafu Kikwete aliyeongozana na Mkewe, Mama Salma Kikwete ameishukuru Serikali kupitia Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kutekeleza takwa hilo la kisheria.

Ameishukuru TBA kwa kukamilisha ujenzi tangu ulipoanza mwaka 2018 na amemshukuru Rais Samia kwa kumkabidhi nyumba hiyo.

Rais Mstaafu Kikwete amempongeza Rais Samia kwa uongozi wake tangu alipopokea kijiti kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais Hayati John Pombe Magufuli kwani nchi imetulia, mambo yanakwenda na watu wana matumaini makubwa nae.

Taarifa kuhusu makabidhiano hayo, imetolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!