Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Siku ya sensa ni mapumziko
Habari MchanganyikoTangulizi

Siku ya sensa ni mapumziko

Spread the love

HATIMAYE Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia tarehe 23 Agosti, 2022 iwe siku ya mapumziko ili Watanzania wawepo majumbani na waweze kuwapokea makarani wa sensa na kutoa maelezo sahihi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Uamuzi huo umekuja siku chache baada ya Kamisaa wa Sensa 2022, Anne Makinda kutoa ufafanuzi kwamba siku hiyo ya sensa tarehe 23 Agosti 23 mwaka huu, haitakuwa siku ya mapumziko badala yake kila mmoja ataendelea na shughuli za kimaendeleo .

Akizungumza katika Kongamano la viongozi wa dini pamoja na kuzindua tangazo la umuhimu wa ushiriki wa sense tarehe 3 Agosti, 2022, Makinda ambaye pia Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri alisema tarehe 23 itakuwa siku maalum ya kuhesabiwa lakini itaendelea taratibu za kuhesabu madodoso hadi tarehe 28 agost mwaka huu.

“Siku hii sio ya mapumziko kuna mtu nilimsikia akisema ni siku ya mapumziko hapana… kila mmoja ataendelea na shughuli zake ila atakuwa ameacha taarifa zake katika makazi ambayo alikuwa amelala siku ya zoezi la sensa” alisisitiza Makinda.

Hata hivyo, katika taarifa iliyowekwa kwenye akaunti za Ofisi ya Waziri Mkuu na msemaji mkuu wa serikali kwenye mtandao wa Twitter zimebainisha kuwa siku hiyo itakuwa ni ya mapumziko.

“Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Alhamisi amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia tarehe 23 Agosti 2022 iwe siku ya mapumziko ili Watanzania wawepo majumbani na waweze kuwapokea makarani wa sensa na kutoa maelezo sahihi”.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!