Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Shule iliyoshika mkia Sengerema, yazinduka
Elimu

Shule iliyoshika mkia Sengerema, yazinduka

Spread the love

 

SHULE ya Sekondari ya Kome, iliyopo Buchosa, Wilaya ya Sengerema, Mkoani Mwanza, iliyokuwa ikishika nafasi ya mwisho kwa matokeo mabovu ya katika wilaya hiyo, imezinduka. Anaripoti Mwandish Wetu, Mwanza … (endelea).

Kome iliyokuwa na matokeo mabovu ya Kidato cha Pili na Nne katika mitihani ya kitaifa kwa miaka mitatu fululizo (2017, 2018 na 2019), sasa imefaulisha kwa asilimia 88 Kidato cha Nne na asilimia 97 Kidato cha Pili mwaka 2020.

Imeelezwa, shule hiyo ni miongoni mwa shule 20 za sekondari ziliko katika Halmashauri ya Buchosa, zilizokuwa na matokeo mabaya kwa miaka mitatu mfululizo kutokana na usimamizi mbovu.

Bruno Sangwa, Ofisa Elimu Sekondari katika Halmashauri ya Buchosa, alifanya mabadiliko ya uongozi wa shule hiyo kwa kumuhamisha aliyekuwa mkuu wa shule hiyo, Lukas Lupimo na kuikabidhi kwa mkuu mpya, Dunua Luhula.

Mwaka 2020, shule hiyo Kidato cha Nne imeshika nafasi ya 14 Kati ya shule 20, amba kimkoa ikishika nafasi 195 ya Kati ya shule 241. Katika matokeo ya Kidato cha Pili, imeshika nafasi ya tisa kati ya shule 20.

Shule hiyo ina wanafunzi 1026, walimu 15, vyumba vya madarasa 11 ambapo mahitaji ni vyumba 23 pungufu ikiwa vyumba 12.

Luhula ambaye ndio mkuu wa shule hiyo kwa sasa, aliyehamishiwa hapo tarehe 11 Februari 2020 amesema, tatizo lilikuwa kutowajibika kwa walimu.

“Kuanzia mwaka 2021, mipango yetu ni kuhakisha shule hiyo inashika nafasi za juu kiwilaya na kimkoa, na kuhakikisha tunatokomeza ziro, ” amesema Luhula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!