KIONGOZI wa chama cha upinzani nchini Kenya cha ODM, Raila Odinga amepimwa na kukutwa na maambukvirusi vya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Raila ambaye ni waziri mkuu mstaafu, alifanyiwa vipimo kadhaa Jumanne ya hiki hii katika Hospitali ya Nairobi, baada ya kulalamika, kutojisikia vizuri.
Jana Alhamisi tarehe 10 Machi 2021, Dk. David Oluoch-Olunya, daktari wa Raila (76), alitoa taarifa kwa umma kuhusu majibu ya vipimo akisema, Raila ameyapokea vyema majibu na anaendelea na matibabu katika hospitaloi hiyo.
Raila amekuwa kiongozi wa kwanza ngazi ya juu wa Kenya, kupimwa na kukutwa na maambukizi hayo.
Leave a comment