KATIBU wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, amemtaka Rais Samia Suluhu Hassan, aanze kuwashughulikia vigogo waliohusika na vitendo vya ubadhirifu wa fedha na mali za umma, vilivyoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Akizungumza jijini Dar es Salaam, leo tarehe 22 Aprili 2023, Sheikh Ponda, amesema kuna baadhi ya hatua zinapaswa kuchukuliwa mara moja kabla yakusubiri maazimio ya Bunge yanayitarajiwa kutolewa Novemba mwaka huu.
“Katika tukio la ripoti ya CAG, tunamshauri Rais achukue hatua zaidi hasa kwa yale mambo ambayo hayahitaji kusubiri hatua za bunge. Kwa mfano suala la kuundwa kwa Tume Huru ya Kumchunguza aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), hilini mamlaka ya Rais,” amesema Sheikh Ponda.
Katika hatua nyingine, Sheikh Ponda amelitaka Bunge lisikawie kufanyia kazi ripoti hiyo ya CAG kwa mwaka wa fedha wa 2021/22.
“Tunashauri Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutochelewesha shughuli za Kamati za Bunge zinazohusika na Usimamizi wa Fedha za Umma ili wananchi waone kuwa wawakilishi wao wanafanyia kazi masuala mazito yanayowahusu,” amesema Sheikh Ponda.
Aidha, Sheikh Ponda ameshauri suala la maadili liwe ajenda kuu ya ujenzi wa taifa, huku akihimiza watendaji wa mamlaka za umma wapewe dhamana kwa kigezo kikuu cha maadili.
Ukweli ni ukweli ndaima..! Cag alichokitoa kifanyiwe kazi, tuone kipi kinaendelea