Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Shehena ya sigara bandia za Bil. 1.8/- kutoka DRC yakamatwa Shinyanga
Habari Mchanganyiko

Shehena ya sigara bandia za Bil. 1.8/- kutoka DRC yakamatwa Shinyanga

Spread the love

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA), Kanda ya Ziwa Magharibi imekamata shehena ya sigara bandia zenye thamani ya Sh 1.8 Bilioni katika mkoa wa Shinyanga zikitokea nchini Congo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga … (endelea)

Kwa mujibu wa taarifa kutoka TMDA, ofisi ya Kanda ya ZiwaMagharibi ilipokea taarifa ya kontena lenye bidhaa za tumbaku lililozuiliwa katika ofisi ya TRA Shinyanga na baada ya kwenda kuzikagua ikabainika kuwa sigara hizo ni bandia.

Taarifa hiyo iliyotolea leo Jumatano tarehe 28 Septemba, 2022 imeeleza kuwa shehena hiyo ilikuwa na jumla ya makasha 2200 yenye uzito tani 13.2.

“Makasha hayo yana uzito wa tani 13.2 kazi hii tulishirikiana kwa karibu sana na MCIE, lakini cha kujiuliza zimepitaje mipakani na tunao wakaguzi huko? Hatua zaidi zinaendelea kuchukuliwa na mzigo huu umezuiliwa,” amesema Gaudensia Simwanza Meneja wa Kitengo cha Uhusiano TMDA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!