Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa IGP, DCI Kenya wajiuzulu, Rais ataja sababu
Kimataifa

IGP, DCI Kenya wajiuzulu, Rais ataja sababu

Spread the love

 

RAIS wa Kenya, Dk. William Ruto jana tarehe 27 Septemba, 2022 amemteua Japhet Koome kuwa Inspekta Jenerali mpya wa Jeshi la polisi nchini humo kuchukua nafasi ya Hilary Mutyambai. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa Rais Ruto, hatua hiyo imetokana na ombi la kujiuzulu la Hilary Mutyambai kutokana na kile alichosema ni matatizo ya kiafya.

Baada ya uteuzi huo jina laKoome litapelekwa bungeni ili kupigwa kura na kuidhinishwa.

Mutyambai ambaye alikuwa amebakisha miezi sita kustaafu, hajaripoti kazini tangu mwezi Agosti kwa kile kilichosemekana kuwa matatizo ya kiafya.

Wadhifa wake ulikuwa ukishikiliwa na Noor Gabow, ambaye alikuwa akipigiwa upatu kuteuliwa kuchukua mahali pa Mutyambai.

Rais Ruto pia alitangaza kujiuzulu kwa Mkurugenzi wa Idara ya Kuchunguza Uhalifu (DCI), George Kinoti, na kusema Idara ya Huduma za Polisi itamteua mrithi wake karibuni.

Wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa tarehe 9 Agosti, 2022 mrengo wa Kenya Kwanza unaoongozwa na Rais Ruto ulimlaumu Mutyambai kwa kile ulichosema ni kukubali polisi kutumiwa kisiasa.

Kinoti naye alilaumiwa kwa madai ya kutumiwa na serikali ya Rais Uhuru Kenyatta kuwahangaisha waliokuwa wakimuunga mkono.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!