Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yadai kumaliza mgogoro wa ardhi Handeni, Kilindi
Habari za Siasa

Serikali yadai kumaliza mgogoro wa ardhi Handeni, Kilindi

Eneo la mpaka wa Kiteto na Kilindi
Spread the love

SERIKALI imemaliza mgogoro wa ardhi kati ya Halmashauri ya Handeni na Kilindi, kwenye eneo la Bondo, uliodumu kwa miaka kadhaa. Anaripoti Jemimah Samwel, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dk. Festo Dugange, leo tarehe 9 Novemba 2023, bungeni jijini Dodoma, akijibu swali la Mbunge wa Handeni Mjini, Reuben Kwagilwa (CCM) aliyehoji lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka kati ya Handeni na Kilindi, ili kuepusha migogoro inayoendelea kila siku.

Dk. Dugange amesema mgogoro huo umemalizika kufuatia maelekzo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Waziri Kindamba, kwenye kikao kilichofanyika tarehe 23 Julai mwaka huu.

Katika hatua nyingine, Dk. Dugange amesema timu ya watalaam wa ardhi, wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya na viongozi wa wilaya hiyo, walikutana tarehe 8 na 9 Oktoba 2021, kwa ajili ya kupitia tangazo la Serikali la kuhakiki idadi ya watu na upatikanaji wa huduma za kijamii.

“Nitoe wito kwa mkurugenzi wa halmashaurikutoa elimu kwa  wananchi juu ya umuhimu wa uhifadhi wa misitu, kuheshimu mpaka ulioanishwa kutokana na tafsiri ya tangazo la serikali. kurekebisha usajiri wa shule za msingi Gondo na Kalakwio ili zisomeke ndani ya wilaya husika,”amesema Dk. Dugange.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za Siasa

Rais Samia asamehe wafungwa 2,244

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewasamehe wafungwa 2,244, huku akiwabadilishia...

error: Content is protected !!