Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yadai kumaliza mgogoro wa ardhi Handeni, Kilindi
Habari za Siasa

Serikali yadai kumaliza mgogoro wa ardhi Handeni, Kilindi

Eneo la mpaka wa Kiteto na Kilindi
Spread the love

SERIKALI imemaliza mgogoro wa ardhi kati ya Halmashauri ya Handeni na Kilindi, kwenye eneo la Bondo, uliodumu kwa miaka kadhaa. Anaripoti Jemimah Samwel, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dk. Festo Dugange, leo tarehe 9 Novemba 2023, bungeni jijini Dodoma, akijibu swali la Mbunge wa Handeni Mjini, Reuben Kwagilwa (CCM) aliyehoji lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka kati ya Handeni na Kilindi, ili kuepusha migogoro inayoendelea kila siku.

Dk. Dugange amesema mgogoro huo umemalizika kufuatia maelekzo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Waziri Kindamba, kwenye kikao kilichofanyika tarehe 23 Julai mwaka huu.

Katika hatua nyingine, Dk. Dugange amesema timu ya watalaam wa ardhi, wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya na viongozi wa wilaya hiyo, walikutana tarehe 8 na 9 Oktoba 2021, kwa ajili ya kupitia tangazo la Serikali la kuhakiki idadi ya watu na upatikanaji wa huduma za kijamii.

“Nitoe wito kwa mkurugenzi wa halmashaurikutoa elimu kwa  wananchi juu ya umuhimu wa uhifadhi wa misitu, kuheshimu mpaka ulioanishwa kutokana na tafsiri ya tangazo la serikali. kurekebisha usajiri wa shule za msingi Gondo na Kalakwio ili zisomeke ndani ya wilaya husika,”amesema Dk. Dugange.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!