Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Muhongo ataka Serikali ibuni miradi kufuta umaskini
Habari za Siasa

Muhongo ataka Serikali ibuni miradi kufuta umaskini

Prof. Sospeter Muhongo, Mbunge wa Musoma Vijijini
Spread the love

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, ameshauri mipango mbalimbali inayowekwa na Serikali, ijielekeze katika utekelezaji miradi ya kufuta umasikini nchini. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Prof. Muhongo ametoa ushauri huo leo tarehe 9 Novemba 2023, bungeni jijini Dodoma, wakati anachangia mapendekezo ya mpango wa maendeleo wa taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali 2024/25 na mwongozo wa maandalizi ya mpango na bajeti ya Serikali kwa mwaka ujao wa fedha.

Mbunge huyo wa Musoma Vijijini mkoani Mara, amesema takwimu za hali ya umasikini nchini, zinaonyesha kwamba, asilimia 18.7 ya watanzania wako chini ya mstari wa matatizo ya chakula, huku asilimia 35.7 wakiwa chini ya mstari wa matumizi ya kawaida, huku hali ya umasikini kwa nchi nzima ni asilimia 13.

Prof. Muhongo amesema ili Serikali iweze kuondoa umasikini, inabidi iongeze nguvu katika sekta ya mifugo, madini, uvuvi, utalii na miundombinu ya barabara.

“Kwa hiyo mipango yetu ijielekeze kwenye miradi ya kufuta umasikini, ili uchumi wetu ukue kati ya asilimia nane hadi 10, kwanza tujielekezekwenye uchumi wa gesi tatu ikiwemo gesi asilimia na gesi nyingine. Tuwekeze katika madini, kilimo, uvuvi na utalii, hivi vyanzo vipaumbele vya mapato,” amesema Prof. Muhongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!