Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yaagiza uchunguzi “Energy Drinks”
Habari Mchanganyiko

Serikali yaagiza uchunguzi “Energy Drinks”

Spread the love

 

SERIKALI imeiagiza Taasisi ya Taifa ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kufanya uchunguzi dhidi ya vinywaji vya kuongeza nguvu (Energy Drinks), ili kubaini kama vina madhara kiafya kama inavyodaiwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 24 Aprili 2023 na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, kupitia akaunti yake ya Twitter, baada ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), kutoa tahadhari kwa wananchi juu ya matumizi ya vinywaji hivyo ikisema kwamba sio salama.

Ummy amesema uchunguzi wa kisayansi utakapofanyika dhidi ya vinywaji hivyo, utaisaidia Serikali kuchukua hatua stahiki.

“Nimeielekeza Taasisi yetu ya Taifa ya Magonjwa ya Binadamu @NIMR_Tanzania kufanya utafiti zaidi kuhusu suala hili la matumizi ya #EnergyDrink na kutupa ushahidi wa kisayansi ili tuweze kuchukua hatua stahiki,” ameandika Ummy.

Vinywaji hivyo pendwa hasa kwa rika la vijana, vinadaiwa kuwa na visisimuzi vingi ambavyo vinaathiri afya ya binadamu hususan mfumo wa damu ambapo inadaiwa mtu anayetumia yuko katika hatari ya kupata tatizo la damu kuganda.

Hivi karibuni, JKCI ilitoa taarifa iliyoeleza kwamba, imemtibu kijana mwenye umri wa miaka 28, ambaye alipata madhara kiafya baada ya kutumia kinywaji hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!