Serikali kupitia Wizara ya Madini imepanga kununua mitambo 15 ya uchorongaji wa miamba kwa ajili ya utafiti wa kina wa madini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita…(endelea).
Hayo yamebainishwa leo tarehe 25 Septemba 25 2023 na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde wakati akizungumza katika kipindi cha Jambo Tanzania (TBC1) kwenye maonesho ya sita ya teknolojia ya madini yanayoendelea katika viwanja vya EPZ bomba mbili mkoani Geita.
Akielezea kuhusu mkakati wa VISION 2030 Madini ni Maisha na Utajiri, Mavunde amesema kuwa Serikali imejipanga kufanya utafiti wa Madini nchi nzima kwa lengo la kupata taarifa zitakazo weza kufungamanisha sekta ya madini na sekta nyingine za kiuchumi.
Akifafanua hali ya utafiti wa madini amesema mpaka sasa utafiti wa kina umefanyika kwa asilimia 16 tu ambazo taarifa zake ndio zinatumika lengo la Serikali ni kuongeza taarifa kupitia tafiti nyingine ziitakazofanywa na GST.
Mpaka sasa sekta ya madini inachangia asilimia 56 ya fedha za kigeni ambazo zinachangia asilimia 9.1 ya pato la Taifa(GDP) , hii ni kwa utafiti wa 16% uliofanyika , hivyo kufikia 2030 tutakuwa tumefanya utafiti nchi nzima.
Sambamba na hapo Mavunde ameeleza kuwa Wizara ya Madini kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira zitaendeleza juhudi za kutunza mazingira kama Sheria zinavyoelekeza.
Pia Waziri Mavunde ameshiriki zoezi la upandaji miti katika viwanja vya maonesho vya EPZ.
Leave a comment