Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Samia:Bajeti ijayo tutazingatia ujenzi nyumba za walimu
Elimu

Samia:Bajeti ijayo tutazingatia ujenzi nyumba za walimu

Spread the love

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake inafanyia kazi changamoto ya upungufu wa walimu nchini, huku akiweka wazi mpango wake wa kutaka kuwajengea nyumba walioko kazini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Mkuu huyo wa nchi akizungumzia ziarani mkoani Singida,  leo tarehe 16 Oktoba 2023, amesema kwa sasa nchi inakabiliwa na upungufu wa asilimia 40 ya walimu wa shule ya msingi na asilimia 26 wa shule za sekondari.

“Suala hili tunakwenda kulifanyia kazi na nimearifiwa kuwepo uhitaji wa nyumba za walimu, hili tunalijua nataka niwahakikishie bajeti ya mwakani Serikali itajielekeza zaidi kwenye ujenzi wa nyumba za walimu. Tumeanza kujenga lakini ni kweli hazijatosha na walimu wanashindwa kukaa maeneo yao kutokana na upungufu wa nyumba,” amesema Rais Samia.

Akizungumzia maendeleo ya sekta ya elimu, Rais Samia amesema serikali yake inaendelea kupeleka fedha katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi pamoja na uendeshaji wa sera ya elimu bila malipo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!