Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Samia:Bajeti ijayo tutazingatia ujenzi nyumba za walimu
Elimu

Samia:Bajeti ijayo tutazingatia ujenzi nyumba za walimu

Spread the love

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake inafanyia kazi changamoto ya upungufu wa walimu nchini, huku akiweka wazi mpango wake wa kutaka kuwajengea nyumba walioko kazini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Mkuu huyo wa nchi akizungumzia ziarani mkoani Singida,  leo tarehe 16 Oktoba 2023, amesema kwa sasa nchi inakabiliwa na upungufu wa asilimia 40 ya walimu wa shule ya msingi na asilimia 26 wa shule za sekondari.

“Suala hili tunakwenda kulifanyia kazi na nimearifiwa kuwepo uhitaji wa nyumba za walimu, hili tunalijua nataka niwahakikishie bajeti ya mwakani Serikali itajielekeza zaidi kwenye ujenzi wa nyumba za walimu. Tumeanza kujenga lakini ni kweli hazijatosha na walimu wanashindwa kukaa maeneo yao kutokana na upungufu wa nyumba,” amesema Rais Samia.

Akizungumzia maendeleo ya sekta ya elimu, Rais Samia amesema serikali yake inaendelea kupeleka fedha katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi pamoja na uendeshaji wa sera ya elimu bila malipo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuTangulizi

Mwalimu Maganga Japhet asimamishwa kazi kwa utoro

Spread the loveMwalimu Maganga Japhet amesimamishwa kazi na Tume ya Utumishi wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

CEO NMB awataka vijana kunoa ujuzi wao

Spread the loveAfisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewashauri...

Elimu

150 wahitimu Shahada ya Udaktari HKMU

Spread the loveCHUO Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU), kimeiomba serikali...

Elimu

Aliyehitimu udaktari HKMU na miaka 21 atoa siri

Spread the love MHITIMU wa fani ya udaktari ambaye ni mdogo kuwahi...

error: Content is protected !!