Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia: Shughuli za kuleta maendeleo ni hatua
Habari za SiasaTangulizi

Samia: Shughuli za kuleta maendeleo ni hatua

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema shughuli za kuleta maendeleo katika nchi ni hatua na kuwahakikishia wale ambao bado hawajafikiwa na huduma mbalimbali kuwa zitawafikia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma … (endelea).

Mkuu huyo wa nchi amesema maendeleo hayawezi kuja ndani yam waka mmoja au miwili na kuweza kuridhisha watu wote.

Ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 17 Oktoba, 2022, akizungumza na wananchi katika uzinduzi wa barabara ya Kasulu na uwekaji jiwe la msingi wa barabara ya Kasulu Manyovu mkoani Kigoma.

Amesisitiza kuwa maendeleo ni safari, “tumeanza na tunakwenda waliopata maji wamshukuru ambao bado tunawahakikishia watapata, waliopata umeme wafurahie waendelee kufanya kazi, ambao bado umeme uko njiani unakuja, waliopata barabara wafurahie ambao bado barabara zinakuja.”

“Kwahiyo ni hatua kitu kikubwa kwetu ni kuwahakikishia tumetumwa na Chama Cha Mapinduzi  kutekeleza ilani yao na tutaitekeleza jinsi mungu atakavyotujalia jinsi uchumi utakavyoruhusu,” amesema.

Ameeleza kuwa ili Seriklai iweze kutekeleza ni lazima wananchi wachape kazi kwa bidii ili kila mtu awe na mchango kwenye maendeleo ya taifa.

Akizungumzia suala la uhaba wa mbolea katika mkoa huo amesema mahitaji yameongezeka baada ya kuanza kwa utaratibu wa ruzuku na kuwahakikishia kuwa tatizo hilo litatatuliwa ndani ya wiki moja hadi mbili.

“Mawakala Kigoma ni wachache tupeni wiki moja, mbili tunakwenda kuongeza mawakala Kasulu na Kigoma mawaziri watakuwa hapa kuhakiisha mbolea inatoka. Mnafaya vizuri kwenye kujiandikisha lakini kwenye namba mtandao unasumbua kidogo lakini nimeongea na Waziri amenihakikishia wataongeza mawakala na kurekebishaa tatizo la upatikanaji wa namba.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!