RAIS Samia Suluhu Hassan amewataka watanzania wadumishe amani na upendo kuelekea kipindi cha uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Rais Samia ametoa wito huo leo tarehe 16 Oktoba 2023, wakati akifungua Daraja la Msingi, lililoko wilayani Mkalama, Mkoa wa Singida.
“Niwaombe kuendelea kutunza amani na utulivu ndani ya nchi yetu, tunaelekea kwenye chaguzi mwakani,” amesema Rais Samia.
Rais Samia amewataka wananchi kuepusha makundi kuelekea chaguzi zijazo “tujitahidi kuepusha makundi, najua kwenye uchaguzi pia una mkono wa Mungu inawezekana unataka sana kuchukua hiyo nafasi lakini Mungu hakukupangia kuchukua hiyo nafasi.”
“Kwa hiyo unapokosa tusianze kutengeneza makundi tukaanza kubomoa chama chetu tukafanya maendeleo yasipatikane tukaanza kufanya chuki, hapana huko tusifikie niwaombe sana dumisheni umoja wenu upendo na mshikamano tufanye chaguzi zetu vizuri zitupe sura chaguzi unaofuata,”amesema Rais Samia.
Mkuu huyo wa nchi amewataka wananchi kuwachagua viongozi watakaowatumikia.
“Tutakuwa na chaguzi za serikali za mitaa, niwaombe sana ndugu zangu kwenye jambo hili moja kuweka watu watakaowatumikia, msiende kuweka kwa watu watakaopitisha watu wengine, kama mnachagua watu katika uchaguzi ule wekeni watu ambao mnajua watakuja watutumikie wa Mkarama,”amesema Rais Samia.
Leave a comment