MKUU wa Mkoa Kilimanjaro, Nurdin Babu ametoa wiki mbili kwa kamati ya ujenzi ya Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD), maabara na nyumba ya mtumishi katika zahanati ya Naibili wilayani Siha mkoani humo kuhakikisha unakamilika. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Babu ameyasema hayo leo Ijumaa akiwa kwenye ziara wilayani kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo inatekelezwa na Serikali.
Amesema Serikali imeroa zaidi ya Sh 271 milioni lengo wananchi wapate huduma za afya kwa wakati hivyo hayupo tayari kuona ujenzi huo unasuasua na kuagiza kituo hicho kijegwe usiku na mchana.
“Viongozi wote katika nafasi zao kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Siha wajue mradi wowote unaotekelezwa katika sekta yake wahakikishe wanausimamia kwa ukaribu na unamalizika ukiwa na viwango vya hali ya juu,” amesema.
Leave a comment