Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemuaga Rais wa Romania, Klaus Iohannis baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi nchini leo tarehe 19 Novemba 2023 Ikulu jijini Dar es salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Pamoja na Rais Samia viongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali wameshiriki kumuaga kiongozi huyo ambao ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk.
Viongozi wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila pamoja na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.
Leave a comment