Tuesday , 21 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wanawake Afrika wampa tuzo ya heshima Balozi Mongela
Habari za Siasa

Wanawake Afrika wampa tuzo ya heshima Balozi Mongela

Spread the love

Wito umetolewa kwa wanawake kujiamini na kujipambanua kitaifa na kimataifa kwenye kusimamia ajenda za maendeleo yenye usawa wa kijinsia na kupinga ukatili wa kijinsia na kwa watoto. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dk. Dorothy Gwajima ametoa wito huo wakati wa hafla ya kumkabidhi, Balozi Dk. Getrude Mongella tuzo ya heshima, iliyofanyika jijini Dar Es Salaam Novemba 18, 2023.

Tuzo hiyo iliyotolewa na Umoja wa Wanawake wa nchi Huru za Afrika (PAWO-Africa) tarehe 31 Julai 2022 nchini Namibia, lengo lake ni kutambua mchango wa Balozi Getrude kwenye uongozi wa ngazi mbalimbali za Kimataifa ikiwemo kuwa rais wa utetezi wa wanawake Afrika na rais wa kwanza wa Bunge la Afrika.

Vilevile, Balozi Getrude amekuwa Mshauri Mwandamizi na Katibu Mtendaji wa Kamisheni Uchumi ya Afrika katika masuala ya Jinsia, Mlezi wa Asasi za Kiraia zisizo za Kiserikali pamoja na kusimamia Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya Wanawake Jijini Beijing nchini China Septemba, 1995.

Dk. Gwajima amempongeza Balozi Getrude kwa ujasiri na uthubutu wake kwenye kutoa mchango wake kwa maendeleo ya wanawake na kuhimiza kuwa, mafanikio haya yakawe chachu kwa Wanawake wengine wote kujiamini kusimamia ajenda za maendeleo ya wanawake.

Aidha, Dk. Gwajima amewahakikishia Wanawake kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan tayari ameweka mazingira mazuri kwa Wanawake wote wenye mchango kwenye safari ya maendeleo yenye usawa wa kijinsia kuendelea kusimama kwenye nafasi zao ikiwemo, kwenye kutokomeza ukatili wa kijinsia na kwa watoto.

Kwa upande wake Balozi Getrude ameshukuru kwa kutambuliwa kwake ambapo amesema, utambuzi huo ni kwa ajili ya wanawake wote walioshiriki kupigania haki za wanawake tangu kuundwa kwa PAWO mwaka 1965.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawale Tanzania (CWT) Mary Chatanda amempongeza Balozi Getrude na kutoa wito kwa Wanawake wote kuunganisha nguvu na kuelekeza juhudi zao kwenye kupambana kutokomeza ukatili wa kijinsia na kwa Watoto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yanawa mikono fidia Kimara-Kibamba

Spread the loveSERIKALI imewataka waathiriwa wa bomoabomoa ya upanuzi wa barabara ya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Geita, Mwanza waongoza kwa mbwa

Spread the loveNaibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Alexander Mnyeti amesema taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 25,039, taasisi 65 wahamia Dodoma

Spread the loveSerikali imesema hadi sasa, jumla ya watumishi 25,039 kutoka Serikali...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Balozi Nchimbi aonya maofisa utumishi kuacha uonevu

Spread the loveKatibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel...

error: Content is protected !!