Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi na utenguzi uteuzi wa Catherine Michael Mashalla, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).
Pia amemteua Jaji Winfrida Beatrice Korosso kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT). Jaji Korosso ni Jaji wa Mahakama ya Rufani.
Katika taarifa iliyotolewa leo Alhamisi na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunus imesema Rais Samia amemteua Bibiana Joseph Kileo kuwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.
Kabla ya uteuzi huu Kileo alikuwa Mkuu wa Mashtaka Mkoa (RPO), Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Mwanza.
Amemteua Alice Edward Mtulo kuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali. Kabla ya uteuzi huu, Mtulo alikuwa Mkurugenzi wa ldara ya Menejimenti ya Kesi na Udhibiti Ubora, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.
Leave a comment