WAKULIMA wa karafuu visiwani Zanzibar, wametakiwa kuacha kuuza kwa magendo zao hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus, wito huo ameutoa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 9 Januari 2024, alipozindua jengo la Kitega Uchumi la Zanzibar State Trade Cooperation (ZSTC), lililopo Chakechake kisiwani humo.
Rais Samia aliahidi kwamba serikali italeta wawekezaji wa karafuu ili kuimarisha mnyororo wa thamani wa zao hilo katika soko la dunia.
“Rais Samia amewataka wakulima wa karafuu kuacha kuchepusha na kuuza kwa magendo zao la karafuu. Pia, amewataka wakulima kuendelea kulima karafuu kwa wingi na kwa tija zaidi ili kuongeza uzalishaji katika sekta ya kilimo na kuinua uchumi wa buluu,” imesema taarifa ya Yunus na kuongeza:
“Vilevile Rais Samia amesema serikali itaendelea kutafuta fursa za kuongeza tija na uzalishaji bila kuathiri viwango na thamani ya karafuu katika soko la kimataifa. Kwa upande mwingine ametoa wito wa ZSTC kutatua kero za wakulima pamoja na kuwa na kanzidata ili kutunza kumbukumbu za zao hilo na wakulima zitakazowezesha kuratibu mipango endelevu.”
Leave a comment