Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5

Screenshot
Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amewasili nchini Uturuki kwa ziara ya kitaifa yenye lengo la kukuza uhusiano wa diplomasia ya siasa, uchumi na biashara kati ya nchi hizo mbili. Anaripoti Gabriel Mushi, Ankara – Uturuki…(endelea).

Rais Samia ambaye ameambatana na ujumbe wa wafanyabiashara zaidi ya 100 pamoja na waandishi wa habari, amewasili jijini Ankara nchini humo saa 10:00 za jioni na kupokewa na viongozi mbalimbali Serikali ya Uturuki pamoja na Tanzania.

Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba, Rais Samia anafanya ziara hiyo  ya siku tano (tarehe 17-21 Aprili)  baada ya Rais wa Uturuki, Tayyip Erdogan kumpa mwaliko wa kutembelea nchini humo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Waziri wa Familia na Huduma za Jamii wa Uturuki Mahinur Ozdemir Goktas mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ankara Esenboga nchini Uturuki kwa ajili ya ziara rasmi tarehe 17 Aprili 2024.

“Nchi ya Uturuki ni moja nchi  ipo kwenye kundi la nchi 20  wanaofanya vizuri hivyo tunajua ziara hiyo itakuwa ya  kimkakati nchini kwetu,” alisema Makamba.

Alisema kuwa lengo lingine la kufanya ziara hiyo ni kupata mtaji na teknolojia ambao nchi ya Uturuki wanayo , kupata masoko ya bidhaa ambayo yapo nchini humo na kupata wawekezaji kwa lengo la kuwekeza nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!