WANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara, kitendo kinachoimarisha shughuli zao za kiuchumi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara…(endelea).
Pongezi hizo zimetolewa hivi karibuni na baadhi ya wananchi wa Mtwara, baada ya Rais Samia kumalizia ziara yake katika mikoa ya kusini.
Dereva wa daladala zinazosafirisha abiria kutoka Soko Kuu hadi Naliendele, Alex Luka amesema baada ya barabara ya Mtwara-Newala-Masasi, kuboreshwa imewasaidia kuondokana na changamoto ya vyombo vyao kuharibika mara kwa mara, pamoja na kuokoa muda.
“Uboreshaji wa hii barabara unatusaidia kupita katika majira yote sababu mwanzoni ilivyokuwa rough road wakati wa masika ilikuwa haipitiki na vyombo vyetu kuharibika. Lakini Sasa hivi imetengenezwa tunaitumia vizuri na tunamshukuru Rais Samia kwa hili,” amesema Luka.
Naye dereva wa bodaboda, Mohamed Mfaume, amesema “tunamshukuru Rais kwa kutuboreshea barabara hii maana miundombinu ya mara ya kwanza ilikuwa mibovu tukawa tunapata shida hususan wakati wa masika barabara haipitiki mvua ikinyesha tunawarushia matope abiria lakini Sasa hivi tunapita vizuri.”
Kwa upande wake Inno Mayunga, amesema baada ya barabara hiyo kurekebishwa, wanaokoa muda wa kusafirisha abiria.
“Ujenzi wa barabara hii ni fursa kwetu madereva wa bodaboda sababu tunatumia muda mfupi kumfikisha abiria anakotaka kwenda tofauti na ilivyokuwa nyuma sababu ilikuwa mbovu. Tunamshukuru Rais Samia kwa hili,” amesema Mayunga.
Leave a comment