Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA
Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the love

ALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald Kusaya ameteuliwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari hii leo tarehe 16 Machi 2023 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, imeeleza kuwa Rais Samia pia amemteua Ally Gugu kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma.

Gerald Kusaya aliyeteuliwa kuwa Katibu Tawala mkoa wa Rukwa.

Kabla ya uteuzi huo, Gugu alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara huku Tixon Nzunda akiteuliwa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro, akichukua nafasi ya Willy Machumu ambaye amestaafu.

Aidha, Rais amemhamisha Fatuma Manga kutoka Mkoa wa Dodoma kwenda kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Singida, akichukua nafasi ya Dorothy Mwaluko ambaye amestaafu.

Rashid Mchata ametolewa Mkoa wa Rukwa kwenda kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Pwani akichukua nafasi ya Zuwena Jiri ambaye amehamishiwa Mkoa wa Lindi akichukua nafasi ya Ngussa Samike aliyepangiwa kazi nyingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

Habari za Siasa

Ataka vifungu vinavyowabana vijana kugombea uongozi viondolewe

Spread the love  MWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama cha ACT-Wazalendo,...

error: Content is protected !!