Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA
Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the love

ALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald Kusaya ameteuliwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari hii leo tarehe 16 Machi 2023 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, imeeleza kuwa Rais Samia pia amemteua Ally Gugu kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma.

Gerald Kusaya aliyeteuliwa kuwa Katibu Tawala mkoa wa Rukwa.

Kabla ya uteuzi huo, Gugu alikuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara huku Tixon Nzunda akiteuliwa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro, akichukua nafasi ya Willy Machumu ambaye amestaafu.

Aidha, Rais amemhamisha Fatuma Manga kutoka Mkoa wa Dodoma kwenda kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Singida, akichukua nafasi ya Dorothy Mwaluko ambaye amestaafu.

Rashid Mchata ametolewa Mkoa wa Rukwa kwenda kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Pwani akichukua nafasi ya Zuwena Jiri ambaye amehamishiwa Mkoa wa Lindi akichukua nafasi ya Ngussa Samike aliyepangiwa kazi nyingine.

1 Comment

  • CANADA Embassy and TACAIDS Here by requesting Trillion USD 56 to finance spread of diseases like HIV, Gonorea and Hapetititis B

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!