Tuesday , 21 March 2023
Home Kitengo Maisha Afya Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari
AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the love

JUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya Bulinda na Butayaibega vilivyopo kata ya Maruku na Kanyangereko wilaya ya Bukoba vijijini mkoani Kagera kutokana na ugonjwa ambao haujafahamika huku dalili zake zikiwa ni kutokwa na damu maeneo mbalimbali ya mwili. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 16 Machi na Mganga Mkuu wizara ya Afya, Prof. Tumaini Nagu, jumla ya watu saba  wanasadikika walipata dalili za homa ya ugonjwa huo. Mbali na homa dalili nyingine zinatajwa kuwa ni kutapika, kutokwa damu maeneo mbalimbali ya mwili na figo kushindwa kufanya kazi.

Mganga Mkuu wa Serikali, Prof. Tumaini Nagu

Taarifa hiyo imesema watu watano kati yao wamefariki na wengine wawili wako hospitali wanaendelea na matibabu.

Amesema mwenendo wa ugonjwa huu unaashiria uwezekano kuwa ni ugonjwa wa kuambukiza.

Amesema Serikali inaendelca kufuatilia kwo karibu kuhusu mwenendo wa ugonjwa huo na kuchukua hatua za kudhibiti ili usisambae.

Ametaja hatua hizo kuwa ni pamoja na; sampuli kutoka kwa wagonjwa na waliofariki zimechukuliwo ili kubaini chanzo na kuthibitisha aina ya ugonjwa huo.

“Ufuatiliaji wa watu wenye viashiria vya ugonjwa kwenye jamii na vituo vya kutoa huduma za afya pamoja na waliotangamana na wagonjwa hao ili kuwapa huduma stahiki za kimatibabu.

“Timu za kitaalamu za kukabiliana na mlipuko ngazi ya mkoa na halmashauri zimetumwa katika maeneo yaliyoathirika na zinaendelea na uchunguzi na hatua za udhibiti.

“Dawa, vifaa na vifaa tiba muhimu vipo katika vituo vya kutolea huduma za afya mkoani Kagera na wagonjwa wanaendelea na matibabu.

“Elimu ya afya inaendelca kutolewa kwa jamii katika mkoa wa Kagera ili kuchukua tahadhari,” amesema Prof. Nagu.

Aidha, amesema wakati Serikali inafuatilia mienendo wa ugonjwa na kuchukua hatua za udhibiti, amewataka wananchi muendelea kuwa watulivu na kuchukua hatua mbalimbali.

Ametaja hatua hizo kuwa  mtu yeyote mwenye dalili za homa, kutapika, kuharisha, kutoka damu na mwili kuishiwa nguvu anashauriwa kuwahi kituo cha kutolea huduma za afya mapema kwa ajili ya uchunguzi na matibabu.

“Kutoa taarifa mapema kwenye kituo cha kutolea huduma kilicho karibu au kupiga simu namba 199 bila malipo endapo utamuona au kukutana na mtu msvenge dalili kamahizo.

“Kuepuka kumgusa mgonjwa au majimaji ya mwili, mate, machozi, damu, mkojo na kinyesi yatokayo kwa mgonjwa au mtu yeyote mwenye dalili hizo,” amesema.

Ameongeza kuwa iwapo itakulazimu kumhudumia mgonjwa kwa dharura, inabidi kuchukua tahadhari ya kujikinga na majimaji yoyote kabla ya kumhudumia.

Inabidi pia kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni au kutumia vitakasa mikono ili kujikinga na magonjwa yote ya kuambukiza.

Pia kepuuka kusalimiana kwa kushikana mikono pamoja na kushirikisha wataalam wa afya katika shughuli za misiba na mazishi katika kipindi hiki.

Aidha, Prof Nagu amewakumbusha watumishi wa afya kuzingatia kanuni za kujikinga na magoniwa ya kuambukiza (IPC) wakati wa kutoa huduma.

Pamoja na mambo mengine amesema Serikali inatoa pole kwa familia zilizoondokewa na wapendwa wao.

“Aidha, nihitimishe kwa kuwaondoa hofu watu wote na kuwaomba kuwa watulivu wakati Wizara inaendelca kufuatilia kwa karibu na kuchukua hatua za udhibiti. Tutaendelea kuwapa taarifa za mwenendo wa ugonjwa huu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Afya

LHRC yapinga kufutwa Toto Afya: Ni ukiukaji wa sheria za watoto

Spread the love  KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimekosoa...

Habari

Tanzania yaungana na nchi 180 kushiriki maonesho ya utalii Ujerumani

Spread the love  TANZANIA imeungana na mataifa 180 duniani kushiriki maonesho makubwa...

Afya

Manesi 7 mbaroni tuhuma za kuwauzia dawa wagonjwa usiku wa manane

Spread the love  JUMLA ya wauguzi/manesi saba wa Hospitali ya Manispaa ya...

error: Content is protected !!