Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ampongeza waziri mkuu mpya Uingereza
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ampongeza waziri mkuu mpya Uingereza

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amempongeza Liz Truss kwa kuchaguliwa kuwa waziri mkuu mpya wa Uingereza na kuchukua nafasi ya Boris Johnson. Anaripoti Apaikunda Mosha, TUDARCo … (endelea).

Rais Samia ametoa pongezi hizo leo tarehe 7 Septemba, 2022 kupitia ukurasa wake wa Twitter kwa kuandika hivi; “Hongera kwako @trussliz kuwa kuchaguliwa kuwa Kiongozi mpya wa chama cha Conservative na Waziri Mkuu wa Uingereza. Tanzania inatarajia kuendeleza urafiki wake wa muda mrefu na Uingereza katika kukuza uhusiano wetu wa kiuchumi na kidiplomasia.”

Truss amechukua nafasi ya Johnson aliyewasilisha rasmi barua ya kujiuzulu kwake kwa Malkia Elizabeth II katika eneo lake la Balmoral huko Scotland na malkia kumteua Truss kuwa waziri mkuu.

Truss mwenye umri wa miaka 47 anakuwa mwanamke wa tatu kuongoza nchi hiyo na waziri mkuu wa nne wa Uingereza katika kipindi cha miaka sita.

Truss alishinda katika kura ya ndani ya chama Jumatatu wiki hii na kumshinda Waziri wa zamani wa Fedha, Rishi Sunak.

Baada ya ushindi wake kutangazwa, Truss aliuambia mkutano wa chama hicho; “Nilifanya kampeni kama M-Conservative na nitawaongoza kama M-conservative”.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!