Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ampongeza Tshisekedi kuchaguliwa tena DRC
Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza Tshisekedi kuchaguliwa tena DRC

Spread the love

RAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza Rais Mteule wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC), kwa kuchaguliwa tena kuliongoza taifa hilo baada ya kumaliza muhula wake wa kwanza aliouanza 2018 hadi 2023. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Mkuu huyo wa nchi amekuwa kiongozi wa kwanza wa nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), kutoa salamu za pongezi kwa Tshisekedi, baada ya jana Jumapili kutangazwa mshindi wa kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu wa DRC uliofanyika tarehe 20 Disemba mwaka jana.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter tarehe 31 Disemba 2023, Rais Samia aliahidi kumpa ushirikiano Rais Tshisekedi katika kuendelea kukuza mahusiano kati ya Tanzania na DRC.

“Pongezi za dhati kwa Rais Tshisekedi kwa kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Natarajia kuendelea kufanya kazi pamoja katika kukuza uhusiano kati ya nchi zetu mbili na watu wetu,” aliandika Rais Samia.

Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na Mkuu wa Tume Huru ya Uchaguzi Congo (CENI), Denis Kadima, Rais mteule Tshisekedi, ameshinda baada ya kupata asilimia 73 za kura zilizopigwa.

Akitangaza matokeo hayo, Kadima amesema aliyekuwa mpinzani wa karibu na Tshisekedi, Moise Katumbi, amepata asilimia 18, wakati aliyeshika nafasi ya tatu, Martin Fayulu akiambulia asilimia Tano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!