RAIS Samia Suluhu Hassan ameonesha kutokukubaliana na mapendekezo ya Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa, kutaka Serikali iangalie uwezekano wa kutoa ruzuku kwa vyama vyote vyenye usajili wa kudumu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Rais Samia amesema kila anayeunda chama anajua atakiendeshaje na kila chama kinakuwa na itikadi yake na kinajua kinaendaje katika kutekeleza majukumu yake.
Rais Samia amesema hayo leo Jumatatu tarehe 21 Machi 2022 baada ya kupokea taarifa ya awali ya kikosi kazi cha kiratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.
“Hivyo vinavyojiendesha vinajiendeshaje? Alihoji Rais Samia na kuongeza, “Unapounda chama cha siasa umejipimaje, utakiendeshaje, unategemea Serikali ikuendeshee chama chako cha siasa? Hapana, ni chama chenu cha siasa mmejiunda sisi itikadi yetu ni hii twendeni tujiendeshe, ruzuku sawa lakini ni kwa wale ambao kweli wanafanyakazi, wapo bungeni wanachapa kazi, unawapa ruzuku ili wajipange wafanye vizuri zaidi lakini hivi vingine je tuviue? Kwahiyo nakuachieni kachemsheni vichwa tuone tunafanya nini na vyama vya siasa na ruzuku.”
Kwa hili UMESHINDA!
Naomba hata kwetu CCM, turudishe viwanja vya michezo kwenye majiji, miji au vijiji.
Tujiendeshe wenyewe bila unyonyaji au ukupe. Tumiliki majengo tuliyojenga kwa fedha zetu na siyo za serikali.
Tujiendeshe wenyewe.
Upo sahihi. Hivi ndivyo vyama vya siasa duniani vnavyojiendesha vyenyewe.
Pia, nchi zenye demokrasia vyama vinaishia ngazi ya wilaya. Hii inasaidia kuweka serikali za mitaa bila chama au siasa isipokuwa maendeleo ya wananchi na haki ya mazingira mazuri.