Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia aagiza benki kupunguza riba kwa wakulima
Habari Mchanganyiko

Rais Samia aagiza benki kupunguza riba kwa wakulima

Spread the love

RAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amezitaka benki zote nchini zinazotoa mikopo, kupunguza riba ili kutowaumiza wakulima wenye nia ya kuendeleza kilimo cha kibiashara. Anaripoti Isaya Temu, TUDARCo…(endelea).

Hayo ameyasema leo tarehe 8 Agosti 2023  alipokuwa akitembelea katika mabanda mbalimbali katika kilele cha sikukuu ya wakulima Nane Nane katika viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya.

Rais Samia ametoa maelekezo akiwa kwenye banda la Benki ya Stanbic ambapo ameitaka benki hiyo pamoja na zingine kupunguza riba kwenye mikopo.

“Mnajua kuna mabadiliko haya ya hali ya hewa, hivyo mkiwawekea wakulima riba kubwa, unamtundika badala ya kumsaidia, kwa hiyo mvua isiponyesha ni kama kusukumia tu kibao afe, umeshamtundika roho yake pale kwenye riba.. kwa hiyo angalieni sera zenu mrudi chini,” amesema Rais Samia.

Wakati huo huo Rais Samia akiwa kwenye banda la NMB alipewa maelezo na mtoa elimu kuwa wao wameshapunguza riba na kufikia asilimi tisa ili kukuza sekta ya kilimo nchini.

Awali, Rais Samia amepokea maelezo kutoka kwa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe walipokuwa katika banda la Stanbic Bank benki hiyo imekuwa ikitoa mkopo wenye riba ya ya kuanzia asilimia 10 kwenda juu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!