Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi awaangukia wafanyabaishara mfumuko wa bei “ tusaidie wananchi”
Habari za Siasa

Rais Mwinyi awaangukia wafanyabaishara mfumuko wa bei “ tusaidie wananchi”

Dk. HUssein Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Daktari Hussein Mwinyi, amewataka wafanyabiashara visiwani humo, kupunguza bei za bidhaa hususan vyakula, ili kuwasaidia wananchi wasiokuwa na uwezo wa kifedha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Rais Mwinyi ametoa wito huo leo Jumanne, tarehe 31 Januari 2023, akizungumza na wafanyabiashara visiwani humo.

Ametoa wito huo baada ya bei za vyakula hasa mchele kupanda bei takribani mara mbili, kutoka wastani wa Sh.1,700 (2020) hadi kufikia 3,000 mwaka huu.

“Leo tunakaribia double price, inaumiza watu pamoja na bei nzuri iliyoko bara tukubali kukosa hiyo faida kwa kipindi hiki, tushushe bei ya ndani,” amesema Rais Mwinyi.

Katika hatua nyingine, Rais Mwinyi amewataka wafanyabiashara hao kuingiza mchele mwingi kwa wakati mmoja ili kudhibiti mfumuko holela wa bei, hususan katika kipindi hiki ambacho mwezi wa Ramadhani unatarajia kuanza.

“Najua kila mtu ana aina yake ya kufanya biashara, msaidiane tushushe mchele kwa wakati mmoja na katika nia moja tu ya kusaidia watu. Biashara inafanyika hata kama faida ni ndogo lakini tulenge kusaidia watu maana Zanzibar mchele ndiyo kila kitu,” amesema Rais Mwinyi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

error: Content is protected !!