Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lataka TBC kuajiri wenye vipaji ili kuvutia watazamaji
Habari za Siasa

Bunge lataka TBC kuajiri wenye vipaji ili kuvutia watazamaji

Dk. Tulia Ackson, Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imelitaka Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), kuajiri watangazaji au wasanii wenye vipaji badala ya kuajiri wenye elimu peke yake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ushauri huo umetolewa leo Jumanne tarehe 31 Januari 2023, bungeni jijini Dodoma na Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, wakati akiwasilisha taarifa ya mwaka ya shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, kuanzia Januari 2022 hadi Januari 2023.

Mtaturu amesema kuwa, kamati hiyo inashauri TBC kuajiri wenye vipaji ili kukidhi ushindani wa soko la sasa.

“TBC kuna watangazaji au wasanii wenye vipaji vizuri lakini hawana sifa za kupata ajira kwa mujibu wa taratibu za Serikali na hali hiyo inasababisha shirika linashindwa kufanya ushindani na makampuni binafsi ya utangazaji ambayo yanazingatia vipaji,” amesema Mtaturu na kuongeza:

“Na kwa kuwa changamoto hiyo inasababisha kupunguza mvuto kwa wananchi ambao huvutiwa na vipaji hivyo, kwa hiyo basi, Bunge linashauri kwamba, Serikali iruhusu shirika la Utangazaji Tanzania – TBC kutoa ajira kwa watu wenye vipaji kulingana na matakwa ya soko.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!