Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kamati ya Bunge yataka kibano wadaiwa sugu kodi majengo ya serikali
Habari za Siasa

Kamati ya Bunge yataka kibano wadaiwa sugu kodi majengo ya serikali

Spread the love

 

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeutaka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), iwachukulie hatua za kisheria wapangaji wake wanaodaiwa malimbikizo ya kodi, kwa kuwa wanakwamisha wakala huo kutekeleza miradi mingine.Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 31 Januari 2023, bungeni jijini Dodoma na Mjumbe wa kamati hiyo, Miraji Mtaturu, wakati anawasilisha taarifa ya mwaka ya shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, kuanzia Januari 2022 hadi Januari 2023.

“Kuna changamoto ya wapangaji wa nyumba za TBA kutolipa kodi kwa wakati, kwa kuwa changamoto ya ulipaji wa kodi kwa wapangaji wa TBA inasabbabisha shirika kupata hasara na kushindwa kutekeleza miradi mingine, Bunge linashauri TBA ifuatilie wadaiwa sugu, iwachukulie hatua za kisheria bila kumuonea mtu aibu,” amesema Mtaturu.

Aidha, Mtaturu amesema kamati hiyo inaiagiza TBA kupeleka taarifa ya utekelezaji wa agizo kwa msajili wa hazina.

Katika hatua nyingine, Mtaturu amesema kamati hiyo inaishauri Serikali itoe fedha kwa TBA kwa wakati ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

error: Content is protected !!