Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Raia 200 wa Tanzania waliokwama Sudan kurejea nchini
Habari za Siasa

Raia 200 wa Tanzania waliokwama Sudan kurejea nchini

Dk. Stergomena Tax
Spread the love

 

SERIKALI imesema kuwa Watanzania 200 waliokwama nchini Sudan wakati huu ambako taifa hilo likiwa kwenye machafuko wapo njiani kurejea nyumbani. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam …(endelea).

Hayo yamebainishwa leo tarehe 25 Aprili 2022 na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Stergomena Lawrence Tax, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Dk. Tax amesema kuwa Serikali ikishirikiana na Bolozi za Jamhuri ya Sudan na Ethiopia imetumia fursa ya makubaliano ya kusitishwa kwa mapigano kwa siku tatu kuanzi tarehe 21 mpaka 23 Aprili, kuondosha raia wa kigeni ili kurejea katika nchi zao.

Amesema kuwa Watanzania hao waliofika katika mpaka wa Ethiopia kwa ajili ya kuelekea kwenye mji wa Adis Ababa kwa lengo kusafiri ambapo tayari ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATC), inawasubiri kuwarejesha nchini.

“Leo wamefika mpakani na Ethiopia na wakifika huko watakuta ndege ya Air Tanzania inawasubiri kuwarudisha Tanzania,” amesema Dk Tax.

Aliongeza kuwa serikali imeona haja ya kuwasaidia raia pia wa ya Uganda, Kenya Burundi ,Zimbabwe,Msumbiji wakiwa kwenye safari moja.

Hata hivyo, baadhi ya raia wa Kenya, tayari wameondolewa nchini Sudan kwa ndege ya jeshi, kutokea uwanja wa ndege wa taifa la Sudan ya Kusini.

Kwa mujibu wa taarifa ya serikali jijini Nairobi, msafara mwingine wa raia wa taifa hilo, Unatarajia kufanyika kesho, ambako mamia ya wananchi wanatarajiwa kusafirishwa kutoka Sudan kuelekea Kenya.

Dk. Tax amemshukuru Rais Samia Suluhu kwa kutoa maelekezo ya maofisa wa kidiplomasia juu ya safari hiyo “muda wowote tutawapokea ndugu zetu watawasili nchini.”

Imeripotiwa zaidi ya watu 400 wameuawa na wengine 3,500 , wamejeruhiwa kwenye mapigano hayo yanayohusisha kikosi cha Rapid Support Force (RSF) na jeshi la serikali .

Wakati huo huo Dk. Tax amekiri kuwa kundi la Waasi la Oromo la nchini Ethiopia wametua nchini Tanzania kwa ajili ya mazungumzo ya kusitisha mapigano nchini mwao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!