Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Makamba: Maji Bwawa la Nyerere yamefikia mita za ujazo bilioni 6
Habari Mchanganyiko

Makamba: Maji Bwawa la Nyerere yamefikia mita za ujazo bilioni 6

Spread the love

WAZIRI wa Nishati January Makamba ameeleza kuridhishwa na kasi ya ujazaji maji Bwawa la kuzalisha Umeme la Mwalimu Nyerere Hydro Power.

Kwa sasa ujazo wa maji umefika mita za ujazo (Cubic Meters) Bilioni 6.  Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).


Amesema zimebaki mita 13 kufikia kiwango cha maji yatakayoweza kuzungusha mitambo ya kufua Umeme.

Makamba ametoa kauli hiyo leo tarehe 25 Aprili 2023 alipofika kwenye mradi wa bwawa hilo lililopo Rufiji mkoa wa Pwani kukagua hatua  na maendeleo mbalimbali yanayoendelea kufanyika kwenye mradi huo.

Amesema kuwa kiwango hicho ni kizuri na kimezidi matarajio yaliyokuwepo awali wakati wa uzinduzi wa ujazaji maji uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan.

“Maendeleo ni mazuri ingawa kazi bado ipo. Kwa mujibu wa takwimu, kiwango cha maji yaliongia wiki mbili zilizopita, ni mengi kuliko maji yaliyoleta mafuriko 2019/2020. Hii maana yake ni kwamba kwa neema ya mvua iliyopo kwa sasa, zile athari za mafuriko zilizokuwepo siku za nyuma hazipo tena.


“Bwawa hili limeanza kuzaa matunda tuliyotarajia ikiwemo kudhibiti mafuriko. Kwa sasa ujenzi wa bwawa kwa ujumla uko asimilia 85.06. Wakati Rais Samia anachukua madaraka ya nchi mradi huu ulikua ni asilimia 37″ – Waziri Makamba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!