Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Prof Muhongo ataka ubunifu mitaala mipya ya elimu
ElimuHabari za Siasa

Prof Muhongo ataka ubunifu mitaala mipya ya elimu

Wanafunzi darasani
Spread the love

SERIKALI imetakiwa kuhakikisha  maarifa, ujuzi, uvumbuzi na udadisi vinazingatiwa kwenye mitaala mipya ya elimu ili kupata wahitimu watakaoweza kushindana katika soko la ajira la kimataifa hasa kwenye masuala ya sayansi na teknolojia. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo ulitolewa jana tarehe 8 Februari 2024 na Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, bungeni jijini Dodoma.

Prof. Sospeter Muhongo, Mbunge wa Musoma Vijijini

Mbunge huyo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema ajira zenye uhitaji wa watu ulimwenguni ni zile zinazohusiana na masuala ya sayansi na teknolojia, ikiwemo za ukuzaji program (Software development), uchambuzi wa habari za kisayansi za data (Data scientific information analyst), uchambuzi na usimamizi wa akili bandia (Management analysis artificial intelgence) na uuguzi.

Amesema ili Serikali iandae watanzania watakaofanikiwa kuzipata kazi hizo ni lazima ibadilishe muundo wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH), ili iwe taasisi badala ya tume.

“Nikiangalia ajira ambazo zinapatikana na kazi namba dunia inayotafuta watu ni software development na  manesi unajua COVID-19 walikufa wengi sana hivyo dunia wanatafuta manesi wenye uwezo, hizi ndizo kazi duniani ili tuzipate lazima na taasisi ya sayansi la sivyo hatutavuka,”amesema Prof. Muhongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!