Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya NMB yamwaga vifaa 750 vya kujifungulia Kigamboni
Afya

NMB yamwaga vifaa 750 vya kujifungulia Kigamboni

Spread the love

BENKI ya NMB imekabidhi msaada wa vifaa mbalimbali 750 vya kujifungulia vyenye thamani ya Sh milioni 15.3 ikiwa ni utekelezaji wa dhamira ya benki hiyo kuinua afya ya uzazi katika Wilaya ya Kigamboni. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Vifaa vilivyotolewa na benki hiyo ni pamoja na, pamba kubwa, mpira ya kuzuia uchafu (disposable mackintosh), taulo za kike za wazazi, nyembe za kupasulia, vibana kitovu vya watoto, nguo za watoto, bomba za sindano, nyuzi za kushonea nk.

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam, Dismas Prosper (wa tatu kushoto), akimkabidhi vifaa tiba Katibu Tawala Wilaya ya Kigamboni, Upendo Mahalu (wa tatu kulia) vilivyotolewa na benki hiyo kwa ajili ya kujifungulia akinamama wajawazito katika Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni. Hafla hiyo ilifanyika ijini Dar es Salaam Disemba 13, 2023. Wa pili kulia ni Mstahiki Meya wa Kigamboni, Ernest Ndamo, Mkurungenzi Manispaa ya Kigamboni, Erasto Kiwale (kulia), Meneja Mahusiano Biashara za Benki na Serikali wa Benki ya NMB, Irene Masaki (kushoto), Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Kigamboni, Rehema Kasilima (wa pili kushoto).

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo iliyofanyika Kigamboni jana, Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam, Dismas Prosper alisema msaada huo umekusudia kuunga mkono juhudi za Serikali za kutoa huduma bora za afya ya uzazi huku akisisitiza kuwa msaada huo utachangia ustawi wa watu binafsi kwa ujumla, familia, na jamii ndani ya wilaya hiyo.

Prosper alibainisha kuwa benki hiyo imeipa sekta ya afya kipaumbele kibubwa kwenye mkakati kabambe wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSI) kwani inaamini kuwa afya bora ni chachu ya maendeleo endelevu.

“Benki ya NMB kwa miaka saba sasa imekuwa ikitenga asilimia moja ya faida baada ya kodi (PAT) kufadhili mipango mbalimbali ya maendeleo nchini kama sehemu ya dhamira yetu ya kusaidia maendeleo endelevu katika maeneo ambayo benki yetu inafanya kazi.

Katibu Tawala Wilaya ya Kigamboni, Upendo Mahalu (wa tatu kulia), akipokea vifaa tiba kutoka kwa Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam, Dismas Prosper (wa tatu kushoto), vilivyotolewa na benki hiyo kwa ajili ya kujifungulia akinamama wajawazito katika Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam Disemba 13, 2023. Kulia ni Mkurungenzi Manispaa ya Kigamboni, Erasto Kiwale, Mstahiki Meya wa Kigamboni, Ernest Ndamo (wa pili kulia), Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Kigamboni, Rehema Kasilima (wa pili kushoto) na kushoto ni Mganga Mfawidhi Msaidizi. Jamse Mbapila.

“Leo tunafuraha kukabidhi vifaa vya kujifungulia vyenye thamani ya shilingi milioni 15.3 na tunaamini juhudi zetu zitasaidia sana kuokoa maisha ya mama wajawazito na watoto wao wachanga,” alisema.

Katibu Tawala (DAS) wa Wilaya ya Kigamboni, Pendo Mahalu wakati wa hafla hiyo alisema wilaya yake mapema mwaka huu ilifanya tathmini ya mahitaji kwa mwaka iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Halima Bulembo na kubaini kuwa wilaya hiyo inahitaji vifaa takribani 8,500 vya kujifungulia kila mwaka kwa ajili ya kuhudumia wanawake wajawazito na watoto wao wachanga.

Alisisitiza kwamba msaada uliotolewa na Benki ya NMB umekuja wakati muafaka na kuihakikishia benki hiyo kuwa wilaya yake itatumia ipasavyo vifaa hivyo vilivyotolewa kwa manufaa ya wanawake wote wajawazito wenye uhitaji.

“Kama wilaya, uhusiano wetu na Benki ya NMB umeenda mbali zaidi ya kuwa washirika wa maendeleo kwani benki hii imekuwa bega kwa bega nasi kila tunapoihitaji. Afya bora inahitaji utoaji wa huduma za afya kwa wakati na kwa ufanisi.

“Tunashukuru sana kwa msaada huu na tunaamini vifaa hivi vya kujifungulia vilivyotolewa vitasaidia kuweka tabasamu kwa kina mama wengi wajawazito ambao mara nyingi wanalazimika kuingia gharama za ziada ili kununua vifaa hivi muhimu,” alisisitiza.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni, Dk. Mohammed Mnyau alisema msaada huo utakuwa ukombozi mkubwa kwa wanawake wajawazito wilayani Kigamboni kwa kuwa vifaa vya kujifungulia ni gharama na kuishukuru benki hiyo kwa mchango wake.

Katibu Tawala Wilaya ya Kigamboni, Upendo Mahalu (katikati), akipokea vifaa tiba kutoka kwa Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam, Dismas Prosper (wa pili kushoto), vilivyotolewa na benki hiyo kwa ajili ya kujifungulia akinamama wajawazito katika Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam Disemba 13, 2023. Kulia ni Mkurungenzi Manispaa ya Kigamboni, Erasto Kiwale, Mstahiki Meya wa Kigamboni, Ernest Ndamo (wa pili kulia) na Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Kigamboni, Rehema Kasilima (kushoto).

“Wakati mwingine ukosefu wa vifaa vya kujifungulia unasababisha ucheleweshaji wa utoaji huduma usio wa lazima. Tunaamini kuwa baada ya kupokea vifaa hivi kutoka Benki ya NMB sasa tutawezesha kutoa huduma za papo hapo kwa wanawake wajawazito wenye uhitaji. Kwa wastani, hospitali yetu inapokea kati ya akina mama wajawazito 5000 – 10,000 kila mwaka,” Dk. Mnyau alisema.

Alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo wilayani humo kuendela kuchangia vifaa vya kujifungulia ili kuiwezesha wilaya yake kufikia malengo iliyojiwekea ya kukusanya vifaa 8,500 mwaka huu.

“Hadi leo, tumeweza kukusanya takriban vifaa 3,500 vya kujifungulia hivyo bado tuna upungufu wa vifaa 5,000 ilikufikia lengo letu la kukusanya vifaa vya kujifungulkia 8,500 mwaka huu.

“Napenda kuchukua fursa hii kutoa wito kwa kampuni zote zinazofanya kazi katika Wilaya ya Kigamboni kutungua mkono katika dhamira yetu nzuri ya kuokoa maisha mama na mtoto,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!