Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Kibiti mkoani Pwani kimepata viogozi wapya baada ya kufanyika uchanguzi wa ndani wa chama hicho hapo jana, Jumapili tarehe 2 Oktoba 2022, ambapo Juma Kassim Ndaruke ameibuka kidedea baada ya kumshinda mpinzani wake wa karibu Abdujabiri Malombwa ambaye alikuwa akitetea nafasi hiyo kwa mara ya tatu.
Katika nafasi hiyo ambayo wagombea walikuwa watatu, Ndaruke alishinda kwa kupata kura 428 dhidi ya 385 za Malombwa huku mgombea wa tatu Abdallah Mpili akipata kura 7.
Kuchanguliwa kwa Ndaruke kuna maanisha kuwa ndio atakuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kibiti kwa miaka mitano ijayo (2022-2027).
Akizungumza na Wajumbe wa Mkutano wa chama hicho ngazi ya wilaya ambao ndio walikuwa wapiga kura, Ndaruke alisema kuwa ni fahari kuona wajumbe wakiwapa nafasi za uongozi vijana ndani ya chama.
“Hii inaonyesha ni kwa kiasi ngani CCM ilivyo wekeza kwenye kukuza vijana. Nachukua fursa hii kwanza kumshukuru Mungu, wajumbe pamoja na kila mmoja wetu aliyeshiriki kwenye uchanguzi. Naomba kusema kuwa hapa aliyeshinda sio Ndaruke mbali CCM ndio imeshinda.
“Tunapokwenda kuanza kazi na uongozi upya nataka kukuchukua fursa hii niwaambie kuwa tutaenda kujenga CCM imara yenye dira na ambayo itakuwa na uwezo wa kuisimamia serikali ili kuhakikisha ya kwamba miradi ya maendeleao kwenye wilaya yetu inatekelezwa pamoja na kumalizika kwa wakati,” alisema Ndaruke ambaye pia ni Mwenyekiti wa UVCCM mstaafu wa wilaya hiyo’.
Akizungumza baada ya kukubali matokeo, mpinzani wa karibu wa Ndaruke na ambaye pia alikuwa anatetea nafasi hiyo Malombwa alisema “Nachukua fursa hii kumshukuru Mwenyekiti wetu mpya na kusema kuwa nimekubali ya kuwa nimeshindwa kihalali kabisa. Lazima tukubali kuwa uongozi ni kupokezana vijiti, muda wangu wa utumishi kama Mwenyekiti wa wilaya umemalizika na kwa sasa kijiti namuachia Ndugu Ndaruke’.
Kwenye uchaguzi huo, kulikuwepo na nafasi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Mkoa ambao walioshinda ni Ashura Matimwa na Uwesu Mtandika na nafasi Mkutano Mkuu Taifa ambao walioshinda ni Ally Seif, Khalid Mtalazaki na Rehema Mkumba.
Leave a comment