Friday , 10 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwalimu matatani tuhuma za ubakaji mwanafunzi
Habari Mchanganyiko

Mwalimu matatani tuhuma za ubakaji mwanafunzi

Spread the love

 

MWALIMU Tunu Broun (37) wa shule ya msingi Senjele wilayani Mbozi mkoani Songwe amedaiwa kutokomea kusikojulikana akikwepa mkono wa sheria baada ya  kutuhumiwa kumfanyia ukatili kwa kumbaka mwanafunzi wa darasa la sita mwenye umri wa mika 14 (jina limehifadhiwa). Anaripoti Ibrahim Yassin, Songea (endelea).

Akizungumza leo tarehe 28 Aprili 2023 huku akitokwa na machozi, Babu anayeishi na mtoto huyo Julias Mwambipile amesema tarehe 17 Aprili 2023 asubuhi aliitwa shuleni na Mwalimu Broun ambapo alitii wito na kufika shuleni na kuelezwa kuwa mjukuu wake ni mtoro darasani.

Amesema baada ya kuelezwa tuhuma za mjukuu wake kuwa ni mtoro aliomba msamaha ambapo mwanafunzi huyo alisamehewa na kuruhusiwa kuingia darasani na yeye kurejea nyumbani.

Amesema mwanafunzi alikiri kuwa ni mtoro huku akidai alikuwa anaogopa kuchekwa na wenzake waliokuwa wakimuita jina la mama wa darasa jambo ambalo mwalimu wao aliwaonya.

Babu huyo mesema muda mfupi baada ga kurejea nyumbani alipata taarifa kuwa mjukuu wake amebakwa ndipo walipoenda kwa mwenyekiti wa kijiji.

Amefafanua kuwa tukio hilo la ubakaji lilijiri baada ya mwalimu huyo kumuamuru mwanafunzi huyo kwenda nyumbani kwake ambapo alipofika alianza kumuingilia kinguvu kwa madai ya kumsaidia darasani na kumpa uongozi wa shule, dada mkuu.

“Baada ya kufanyiwa ukatili huo, Mwalimu huyo alimuagiza mtoto huyo kurejea nyumbani lakini kutokana na maumivu makali yaliyomfanya kushindwa kutembea vizuri, msamaria mwema aliyekutana naye njiani alimhoji kisha kumueleza kilichomtokea.

“Msamaria mwema huyo aliamua kumpeleka kwa Mwenyekiti wa kijiji cha Senjele, Juma Shipela ambapo walifanyia mahojiano,”amesema.

Amesema waliamua kwenda shuleni hapo na kukuta mwalimu huyo mtuhumiwa ametokomea kusikojulikana.

Bibi wa muhanga Rose Mwampashi amesema wajukuu zake anawalea kwa taabu na alitegemea mwalimu angekuwa ni msaada kwa watoto ili wafikie ndoto zao za kielimu lakini sasa imekuwa kinyume.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio hilo Kamanda wa polisi mkoani Songwe, Theopista Malya amekiri kuwepo kwa tuhuma hizo za mwalimu kumbaka mwanafunzi wake.

Amesema tayari wamemfungulia jalada la uchunguzi huku wakiendelea kumsaka mwalimu huyo.

Amesema mwalimu huyo alitenda kosa hilo tarehe 17 April mwaka huu nyumbani kwake muda wa mchana huku akitumia mbinu ya kumlaghai kumsaidia kimasomo kutokana na maisha duni aliyonayo.

Malya amesema baada ya mtuhumiwa kutenda kosa hilo, ametoroka na kufunguliwa jalada la uchunguzi namba MWO/315/2023 na pindi atakapokamatwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Natoa wito kwa jamii kuacha vitendo vya ukatili kwa watoto kwani vitendo hivyo vinafifisha ndoto zao.
Aidha, Kamanda Malya amewataka wananchi na jamii yote kwa ujumla kuacha vitendo vyote vya ukatili dhidi ya watoto ambavyo vimezidi kukithiri mkoani Songwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waitara ahoji bungeni mwarobaini mauaji katika mgodi Barick North Mara

Spread the loveMBUNGE wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara, ameitaka Serikali kutafuta...

error: Content is protected !!