Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Musoma Vijijini wafanya harambee posho za walimu, ujenzi wa sekondari
Elimu

Musoma Vijijini wafanya harambee posho za walimu, ujenzi wa sekondari

Spread the love

 

WAKAZI wa Jimbo la Musoma Vijijini, wakiongozwa na Mbunge wao, Profesa Sospeter Muhongo, wamefanya harambee ya kuchangisha fedha za kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya shule mpya ya Sekondari Bwai, mkoani Mara. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Ijumaa tarehe 20 Januari, 2023 na Ofisi ya Mbunge wa Musoma Vijijini, harambee hiyo imefanyika jana tarehe 19 Januari 2023, ikiongozwa na Prof Sospeter Muhongo .

“Harambe imefanyika ya ukamilishaji wa vyumba vitatu vya madarasa, kwa sasa vyumba vilivyokamilika na vinatumika ni vitatu. Ujenzi wa choo kipya chenye matundu manne, kwa sasa kipo choo chenye matundu manane,”

“Ujenzi wa jengo la utawala ambalo msingi wake umekamilika. kwa sasa, ofisi ya walimu ni chumba kimoja cha darasa. Ujenzi ni endelevu, na michango ni endelevu hadi hapo miundombinu muhimu itakapokamilika, ikiwemo, maabara tatu za masomo ya sayansi, maktaba, nyumba za walimu, viwanja vya michezo,” imesema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imetaja michango iliyopatikana katika harambee hiyo ambayo ni endelevu, ikiwemo saruji mifuko 51 iliyotolewa na wananchi pamoja na mifuko mingine 100 iliyotolewa na Prof. Muhongo.

Pia, wananchi walichanga misumari kilo tatu, fedha taslimu kiasi cha Sh. 610,000 na nguvu kazi ya kujenga miundombinu hiyo, huku Prof. Muhongo akichangia mabati bando mbili zenye jumla ya mabati 24.

Kwenye harambee ya kupata walimu, wazazi wamekubali kuchangia Sh. 3,000 kila mwezi, pamoja na kuajiri walimu wa kujitolea kwa posho ya Sh. 200,000 kila mwezi, huku Prof. Muhongo akiahidi kuchangia Sh. 100,000 kwa kila mwalimu kwa mwezi , ambao wako watatu (jumla Sh. 300,000).

Taarifa hiyo imeeleza zaidi kuwa, Prof. Muhongo ametoa makasha manne ya vitabu kwa sekonda hiyo mpya yenye kidato kimoja.

Kwa sasa shule hiyo ina walimu watano akiwemo Mkuu wa Shule, lakini haina walimu wa masomo ya Kingereza, hesabu na fizikia.

Shule ya Sekondari Bwai ina wanafunzi 125 kati ya 153 ambao wanatakiwa kuanza masomo yao ya kidato cha kwanza.

“Vilevile, shule hiyo mpya, iitwayo Bwai Sekondari, itapunguza mirundikano ya wanafunzi kwenye madarasa ya Sekondari ya Kiriba,” imesema taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!