Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Binti wa miaka 17 ajinyonga kisa mzazi mwenzie kugomea matunzo ya mtoto
Habari Mchanganyiko

Binti wa miaka 17 ajinyonga kisa mzazi mwenzie kugomea matunzo ya mtoto

Kitanzi
Spread the love

 

WINFRIDA Mandindile (17), amejinyonga kwa madai ya mzazi mwenzie kugoma kutoa fedha za matumizi ya mtoto wao mwenye umri wa mwaka mmoja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).

Kisa hicho kimetokea hivi karibuni mkoani Iringa, ambapo mama wa marehemu, Agnes Donald, amedai kabla ya binti yake kuchukua uamuzi wa kujinyonga alikuwa anampa malalamiko ya mwanaume huyo ambaye wote walikuwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kihesa, kwamba hataki kumhudumia mtoto wao.

Agnes alidai kuwa, mwanae alipata ujauzito akiwa kidato cha kwanza, wakati mwanaume akiwa kidato cha nne.

Agnes Donald, Mama wa marehemu

“Mimi nilikuwa naye jirani namfariji nikimwambia wanaume waongo na nilikuonya toka ukiwa darasa la saba, nafikiri chanzo cha kuchukua maamuzi hayo ni msigano wa yeye na mwenzake,” amedai Agnes.

Mkuu wa Kituo Kidogo cha Polisi cha Semtema, Cosmas Ngai, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo akisema lilichangiwa na wazazi kutokuwa karibu na marehemu wakati anapitia magumu.

“Inaonekana alikosa ushauri labda angepata ushauri wa kutosha asingechukua uamuzi huo,”amesema Afande Ngai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!