RAIS Samia Suluhu Hassan ameonesha kufurahishwa na utendaji kazi wa balozi wa maji nchini ambaye ni msaani maarufu wa mziki wa kughani mashairi, Mrisho Mpoto na kumtaka kuendelea na kazi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Rais Samia alimteua Mpoto kuwa balozi wa maji wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji jijini Arusha baada ya kuonesha umahiri mkubwa wa kuijua miradi mingi ya maji iliyotekelezwa na Serikali.
Akizungumza leo Jumanne tarehe 22 Machi 2022 kwenye uzinduzi wa mradi wa maji Mlandizi-Chalinze-Mboga, Rais Samia amesema cheo alichopewa Mpoto cha uhandisi kinamfaa kwa namna anavyoijua miradi ya maji.
“Enjinia Mpoto kweli hii title (cheo) inakufaa sana maana nilipopendekeza upewe ubalozi huu nadhani ni mwezi tu tukio lile na leo lakini miradi yote ya Tanzania unaijua endelea baba kuzunguka, endelea kusema,” amesema Rais Samia.
Leave a comment