Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Ukraine kuhutubia Bunge Japan
Kimataifa

Rais Ukraine kuhutubia Bunge Japan

Spread the love

RAIS wa Ukraine, Volodymyr Zelensky kesho Jumatano tarehe 23 Machi, 2022 anatarajiwa kuhutubia Bunge la Japan kwa njia ya mtandao.

Hotuba yake inatarajiwa kuzungumzia mashambulizi ya Urusi nchini mwake, kuomba msaada na uungwaji mkono kutoka kwa mataifa mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Kwa mujibu wa Aljazeera, hotuba ya Rais huyo inatarajiwa kutumia dakika 10 pekee na itaonesha mubashara kupitia vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa.

Rais huyo amepata nafasi hiyo baada ya Waziri Mkuu wa Japan, Fumio Kishida kukubaliana na mpango huo katika kutoa nafasi kwa Ukraine kuendelea kuomba msaada wa kimataifa kukabiliana na vita hiyo.

Tangu vita ianze tarehe 24 Februari, mwaka huu, Rais huyo wa Ukraine amekwishahutubia Bunge la Marekani, Ulaya, Canada na Israel.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!