Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Biashara Mradi wa maegesho ya malori wazidi kuipaisha Tunduma
Biashara

Mradi wa maegesho ya malori wazidi kuipaisha Tunduma

Spread the love

HALMASHAURI ya mji Tunduma wilayani Momba mkoani Songwe imetumia kiasi cha Sh 1.7 bilioni kujenga mradi huo wa maegesho ya malori ili kukabiliana na msongamano wa malori lakini pia kuongeza mapato ya halmashauri hiyo. Anaripoti Ibrahim Yassin…(endelea).

Hayo yamebainishwa leo tarehe 8 Julai 2023 na Afisa mipango wa mji Tunduma, Broun Garigo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri kuhusu ujenzi wa mradi huo.

Amesema baada ya ujemzi wa mradi huo, imewezesha kuwa chanzo kipya cha makusanyo ya mapato ya halmashauri hiyo ambayo kwa mwezi hukusanya Sh 5.9 milioni na kwa mwaka ikiwa ni Sh 70.8 milioni.

Amesema Tunduma ni mji wa kibiashara na asilimia 75 ya bidhaa zinazovuka kutoka bandari ya Dar es salaam husafirishwa kwa malori hadi kuelekea mpaka.

Amesema mchakato wa ujenzi wa mradi huo ulianza mwaka 2021 na sasa umekamilika na kuanza kufanya kazi.

“Ni moja ya vyanzo 35 vya mapato vinavyoiwezesha  Tunduma kukusanya zaidi ya Sh 11 bilioni kwa mwaka na kushika namba mbili kitaifa kwa makusanyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yashiriki maadhimisho Mei Mosi Arusha

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeungana na maelfu ya...

Biashara

Promosheni ya bil 1 kutoka Meridianbet kasino, cheza na ushinde zawadi kubwa

Spread the love  INGIA katika ulimwengu wa zawadi za kushangaza: Jishindie sehemu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

error: Content is protected !!