Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko 127 wahukumiwa usafirishaji haramu wa binadamu
Habari Mchanganyiko

127 wahukumiwa usafirishaji haramu wa binadamu

Spread the love

JUMLA ya kesi 72 za makosa ya usafirishaji haramu wa binadamu zilifunguliwa mkoani Songwe huku watuhumiwa 127 wakihukumiwa baada ya kukutwa na hatia kutokana na biashara hiyo haramu. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Aidha, jumla ya wahanga 892 waliokolewa katika usafirishaji huo haramu ambapo watanzania wengi huenda kutumikishwa nje ya nchini kwa kupitia nchi mbalimbali za mipakani.

Akizungumza na MwanaHALISI Online leo tarej 8 Julai 2023 Katibu Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na usafirishaji haramu wa Binadamu kutoka Wizara ya mambo ya ndani ya nchi, Separatus Fella amesema watuhumiwa hao walikamatwa kwa nyakati tofauti kutokana na ushirikiano mzuri wanaoupata kutoka kwa jamii ya Watanzania pamoja na vyombo  vya dola.

Aidha, Mkurugenzi wa Miradi kutoka Shirika la Tanzania Relief Initiatives (TRI), Damiani Edward amesema wametoa mafunzo katika  mikoa 19 Tanzania Bara na Visiwani ili kukabiliana na biashara hiyo haramu.

Amesema tayari watekelezaji 2000 wa sheria wakiwamo maofisa wa polisi, ustawi wa jamii na wadau wengine,  wamepatiwa mafunzo licha ya uwepo wa uelewa mdogo katika kufanikisha hili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!