Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mjema ‘out’ CCM, Makonda atajwa
Habari za SiasaTangulizi

Mjema ‘out’ CCM, Makonda atajwa

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Sophia Mjema kuwa Mshauri wa Rais masuala ya Wanawake na Makundi Maalum.

Kabla ya uteuzi huu Sophia alikuwa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mwanamama huyo anaweka rekodi ya kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi aliyeshika nafasi hiyo kwa muda mfupi wa miezi tisa na ushee.

Hata hivyo, kabla ya uteuzi wa sasa, Sophia aliibua mijadala kwa wachambuzi wa masuala ya kisiasa baada kudai kwamba Rais Samia anapaswa kuiongoza Tanzania kwa miaka 10 ijayo kuanzoa mwaka 2025.

Mjema alitoa kauli hiyo mkoani Mara wakati akizungumza na wanawake mkoani humo ambapo alisema kwa utendaji na kasi anayoionesha Rais Samia anastahili miaka 10 kuanzia mwaka 2025.

Mbali na kupingwa vikali kuwa ni ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayomtaka Rais kuongoza kwa mihula miwili, tayari wengi wao walikuwa wamebainisha kuwa nafasi hiyo ya kisiasa ndani ya CCM haimtoshi.

Hayo yanajiri wakati CCM ikijipanga kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 na uchaguzi mkuu 2025.

Hata hivyo, kutokana na joto hilo la uchaguzi fununu za Sophia kung’olewa kwenye nafasi hiyo zilianza mapema wiki hii baada ya Rais Samia kuitisha Mkutano wa dharura wq halmashauri kuu ya taifa CCM (NEC) huku aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akitajwa kupeww nafasi ya Sophia.

Makonda ambaye ni mmoja wa wanasiasa machachari ameibua mjadala ndani ya mitandao ya kijamii kutokana na aina ya siasa za mapambano amekuwa akizifanya dhidi ya wapinzani wake ndani na nje ya CCM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!