Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mfanyabiashara Tanga amwangukia Majaliwa zabuni ya Jamhuri Pack ‘Forodhani’
Habari Mchanganyiko

Mfanyabiashara Tanga amwangukia Majaliwa zabuni ya Jamhuri Pack ‘Forodhani’

Mfanyabiashara, Sultan Salim
Spread the love

 

MFANYABIASHARA Sultan Salim wa jijini Tanga, amemuomba Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Kassim Majaliwa, kuingilia kati mchakato wa upatikanaji wa mshindi wa zabuni wa eneo la Jamhuri Pack ‘Forodhani’ jijini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imekuja baada ya mfanyabiashara huyo kudai kudhulumiwa haki yake kutokana na mchakato ulivyofanywa hadi kupatikana mshindi kuna taratibu na kanuni zimekiukwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Salim alisema kinachoonekana wanataka kumnyima haki yake kwa makusudi kwani alistahili kushinda tenda hiyo kutokana na dau kubwa alilotoa.

“Agosti Mosi, mwaka huu niliomba tenda hiyo ya Jamhuri Pack na nashukuru nilishinda kwakuwa dau langu la sh. milioni 2 na mia mbili hakuna ambaye alilifikia siku hiyo ya ufunguzi wa zabuni hiyo,” alisema na kuongeza;

“Lakini chakushangaza Halmashauri ya Jiji la Tanga ilivyofika Agosti 8, mwaka huu wakatoa makusudio ya upangaji na kumtangaza Ali Salim Mohamed kuwa mshindi kwa dau la sh. mil. 2.3 wakati siku ya ufunguzi tenda hiyo alitoa dau la Sh. 1.3 milioni.”

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu,

Alisema anashangaa kuona mpinzani wake kutangazwa ameshinda tenda hiyo wakati siku ya ufunguzi alitoa dau dogo na yeye alitoa kubwa kitu ambacho kinampa maswali mengi bila majibu.

Akifafanua zaidi alisema baada ya sintofahamu hiyo aliandika barua kwenda halmashauri kupinga matokeo hayo pamoja na kuweka zuio lakini majibu yakabaki vile vile.

“Halmashauri ilijibu kwa kutilia mkazo matokeo yao ya awali waliyoyatoa na hata nilipoandika barua ya pili kwao na kuambatanisha na nyaraka zote za mchakato mzima ulivyoanza hadi kunionesha mimi ndiye nilipaswa kuwa mshindi, haikusaidia kitu kwani halmashauri ilikataa kupitia nyaraka zangu,” alisema Salim.

Alisema kutokana na sintofahamu hiyo ndio maana ameamua kukimbilia kwa Waziri Mkuu, Majaliwa akiamini atalifanyia kazi na ukweli kuwekwa wazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!