KATIBU tawala mkoani Songwe, Happiness Seneda, ameupongeza uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Momba kwa kufikisha asilimia 54 ya makusanyo ya fedha. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe … (endelea).
Seneda aliyasema hayo le tare 14 Novemba, 2023 wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani humo ambapo licha ya kukagua miradi mbalimbali pia alitumia nafasi hiyo kuipongeza halmashauri hiyo kwa kufikisha asilimia 54 ukilinganisha na halmashauri zingine.
“Nipo wilayani Momba kukagua miradi nikianzia wilayani Mbozi, miradi ipo vizuri, kasoro zilizopo zirekebisheni, nikupongeze mkurugenzi na timu yako mpo vizuri endeleeni na ushirikiano huo ili msonge mbele “ameema Ras Seneda.
Akipokea pongezi hizo, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Regina Bieda, amesema licha ya kupongezwa watahakikisha wana ongeza jitihada ili wakusanye zaidi.
Ameema katika mwaka wa fedha 2023/2024 walikisia kukusanya Bilioni 1.8, hadi kufikia mwezi Oktoba 30 walifikisha asilimia 54 hali inayowapa matumaini ya kuvuka lengo.
“Katibu tawala nashukuru kwa kutambua jitihada tunazofanya, tutaongeza juhudi zaidi, mafanikio hayo yamekuja kutokana na ushirikiano mzuri kati ya watumishi, madiwani na wananchi,” amesema Bieda.
Ikumbukwe kuwa katibu tawala mkoani humo, yupo kwenye ziara ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye tarafa zote mkoani humo.alianza halmashauri ya Tunduma, Mbozi na sasa yupo Momba.
Leave a comment